Monday, March 16, 2020

HIVI UNAJUA MSAMAHA UNAOKOA MAHUSIANO MENGI SANA

Image may contain: text

MSAMAHA ulikomboa Mahusiano mengi.
MSAMAHA ulijenga NDOA nyingi.
MSAMAHA ulileta AMANI mahala palipokuwa pamekosa TUMAINI.
MSAMAHA ulitengenza FURAHA pale palipokosa TABASAMU.
Na kila aliyeomba MSAMAHA alijitenga na GHADHABU ya aliyemkosea, Ndo maana MSAMAHA una nguvu ya KUJENGA kuliko KUHARIBU
Ukisamehe unajiweka HURU ndani yako, Ukisamehewa unajitenga na UPWEKE ndo maana nikasema MSAMAHA NI DIRA YA WEMA.
Asiyekuwa na MSAMAHA ni mchawi, aliyejaaliwa MSAMAHA ana rehema na ndo maana halisi ya UPENDO๐Ÿ’–
Jifunze kusamehe kwa namna yoyote ya Makosa ama maudhi ili uwe na AMANI MOYONI MWAKO ๐Ÿ’“
Kuna msamaha ambao unakulazimu kusamehe ili kutimiza MAANDIKO ila ukiishajua kwamba unayemsamehe hana UPENDO kwako Basi na ujitenge nae, Maana kusamehe kunawapasa wenye MOYO SAFI.
#Elista_Kasema_ila_Sio_Sheria๐Ÿ‘ฃ


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/03/hivi-unajua-msamaha-unaokoa-mahusiano.html

No comments:

Post a Comment