Kwanza naomba nikwambie jambo moja;
"ALIYEACHWA AMA KUUMIZWA NDIYE ANAYEKUFAA ZAIDI IKIWA NAWE UMEJIPANGA KUINGIA PENZI LENYE FURAHA NA AMANI"
Bwaga manyanga yako chini, Tupa vidumu na vibakuri ili UPEWE UPENDOπ
Hakuna aliyefurahia MAPENZI kwa kumpata mtu FRESH yaani ambaye ndo anayaanza mapenzi⛔ Wala hakuna aliye mwalimu wa mwenzie kwenye MAPENZI ila kila mtu hujifunza mwenyewe kutokana na MAKOSA AMA MAAMUZI YAKEπͺπ½ Tambua kwamba hata Elimu haijengwi na Mwalimu mmoja, Mtu kufikia PHD ni mpaka awe amefunua vitabu vingi, Kuna wakati utajikuta huelewi unachokisoma, lakini unavyoendelea kusoma ndivyo ambavyo UTAJIKUTA UNAELEWAπ Vivyo hivyo issue inayohusu MAHUSIANO/NDOA kwa ujumla na mapana yake huitwa MAPENZI ukomavu wake unaendana na namna ya MAPITO YAKO! Kwani mtu hujifunza kutokana na mwenendo wa uhalisia aliopo, Unaweza kuumiza wengi mwisho wa SIKU AKAJITOKEZA KIBOKO YAKOπ Na hiyo ndo maana ya wewe kutajwa kuwa mwenye PhDπͺπ½
Ni ngumu kuwa kwenye PENZI lililo na FURAHA NA AMANI ikiwa wewe mwenyewe huwezi kumpa FURAHA NA AMANI mwenza wako, Ukiona mtu anafikiria kukuacha ama ukaona matendo yanayoashiria kukuchoka ujue UMEMUONDOA KWENYE UPENDO na ndo maana anajaribu kujikomboa, Nikiri inaweza kuwa HASARA yenu wote ikiwa MTAACHANA MNAPENDANA⛔
Hakuna Malaika kwenye MAPENZI sote tunaishi kwa kuzifuata NAFSI zetu japo huwezi kuwa na Mpenzi wako bila kupitia changamoto, Malezi na maamuzi kila mmoja na yake hivyo linaloweza kuwabeba ni UPENDOπ€πΌ
Ili kupata idadi ya wangapi uliwahi kuwa nao kama wapenzi LALA KITANDANI TAFAKARI PEKE YAKO ukipata majibu inuka ujiangalie n then UJIJIBU MWENYEWE IKIWA KUNA FAIDAππ»♂
Kuna starehe gani KUBADILI radha za wanawake? Je ni utamu ndo unaokupa kuendelea kuutafuta? Ama ni kujua size na kuongeza orodha ya wanawake?
Ingekuwa utamu unalinda MAPENZI wallah FANTA isingekuwa inakinaishaπ€£π€£
Usimtazame mwanamke kwa matamanio kwamba atakuwa MTAMU HUYU Kwani UTAMU HALISI NI KUTOKANA NA VILE WEWE UNASHIRIKI NA MWENZIOπ
Mapenzi yanahitaji utulivu wa akili pamoja na kutomlinganisha mwenza wako na mtu mwingine, Ukipata BUSARA umemlinda mwenza wakoππ»♂
source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/03/aliyeachwa-ama-kuumizwa-ndiye.html
No comments:
Post a Comment