Friday, May 22, 2020

VITA KUBWA BAINA YA MWANAMKE NA MWANAUME KWENYE MAPENZI NI PALE MWANAMKE ANAPOKOSA MAHITAJI YAKE.


UTAMUZAIDIAPP
Ukweli ni kwamba Mwanamke ili afurahie mahusiano aliyopo ni pamoja na KUPATA MAHITAJI YAKE.
Unajua wanaume wengi hawajui namna ya kuendelea kumkamata mtoto wakike japo wanajua kuanza vizuri sana ila kusimamia Mwanzo wao ndo shida, Mwanzo wa MAHUSIANO hakuna Mwanamke anauchukia na pengine ndo Maana Wanawake wakikosa waliyo yatarajia kwa wenza wao huangukia kwenye kutoa nafasi kwa Mwanaume mwingine kwa sababu atakapokuwa anatongozwa ATAPATA ANACHOKIKOSA KWA ALIYE NAE💃
Kwa sasa wanawake wanaamini NI BORA KUANZISHA MAHUSIANO KULIKO KUISHI NA MTU AMBAYE ANAKUUMIZA kwa sababu Mwanzo anakutana na Mwanaume ni rahisi kwake kuweka conditions na Mwanaume asiweze kukataa.
Kila Mwanamke mkubwa na mdogo wanahitaji KUDEKEZWA na ni nafasi nzuri sana kwa Mwanaume kumpata Mwanamke ikiwa ATAMDEKEZA na ndo maana wanaume wanaojua kudekeza HUWA HAWAACHWI NA MWANAMKE ila wao kumuacha Mwanamke.
Ni kweli Mwanzo wa MAHUSIANO huo ndo humjenga Mtu kuwa na shauku ya kuwa na Mtu, Maana hata ukimwambia mtu APANDE GUTA KUKUFUATA KARIAKOO KIPINDI KAMA HIKI NA MAFURIKO YA JANGWANI ATAKUJA KWA WAKATI ila mvulie chupi👙 sasa halafu unaishi GONGOLAMBOTO wallah hawezi kuja tena laa umfuate wewe napo anaweza kukukwepa ISIPOKUWA UWE UNAJUA KUCHEZA SINDIMBA hapo atayafikiria Mauno 😅😅
Wanaume STAREHE yao ni PENZI JIPYA ndo maana unaweza kukuta jamaa ana Mke mzuri Balaa ila sasa kutulia Mmmmh😎
Saa zingine wanawake hamjui kutumia TALENT yenu Mungu kawajaalia, Unajua ukiona Mwanaume hatulii kwanza soma anatatizo gani? Je shauku yake unaweza kuitimiza? Unajua unakuta Mwanaume anapenda kitu fulani na hawezi kumwambia mkewe eti bora akamfundishe KAHABA kuliko mkewe hawa bin adam ni wa ajabu mno, Ni nafasi yako Mwanamke kupambania PENZI hilo ikiwa unalipenda lakini maana siku hizi nanyi hamtabiriki mpo tayari kuteseka eti kisa unamkomoa  wako Kwani bi Dada jamaa ndo anapumuliwa si ni wewe? Mungu amewajaalia UFAHAMU MPANA Basi mfahamu Mwanaume wako ili uweze kukabiliana nae, Hawana ujanja hao ni wadogo kama sisimizi🐜
Unajua wanaume wengi husaliti awapo na UHURU ulopitiliza vivyo hivyo hata Mwanamke kwa maana hiyo USIMUACHE HURU SANA MUMEO uwe kiranja kila mara kumuangalia MATENDO yake, Mwanamke MAKINI hasalitiwi kijinga mpaka Mwanaume atumie GHARAMA kubwa kupata nafasi hiyo, Sasa wewe kaa kama PAMBO uone wenzio wanavyo kumalizia utamu akirudi amechoka na usanii kibao, Wanaume wanafanana UKIMPENDA MMOJA mshike huyo, Tena Mwambie HAPA UMEFIKA na kuondoka mpaka MUNGU APENDE ila kama ni uhuni wako UTAUMALIZIA KWANGU💪


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/05/vita-kubwa-baina-ya-mwanamke-na.html

No comments:

Post a Comment