Friday, May 22, 2020

KILA NDOA INA MALENGO YAKE TATIZO KUU KWA NDOA ZA SASA NI KUTONIA MAMOJA💯


Kabla ya kufikiria NDOA jitafakari;
👉 JE MALENGO YAKO NI YAPI NA JE HUYO UNAYEFIKIRIA KUWA NAE KAMA MWENZA WA MAISHA YAKO YEYE MALENGO YAKE NI YAPI?
Maana halisi ya MWENZA WA MAISHA ni Mtu ambaye lazima Muendane ki mtazamo pamoja na malengo iwe kwa kumbadili yeye afuate upande wako kwani kinyume chake ndo maana NDOA ZIMEKUWA MWIBA kwa sababu Wewe una mlengo wako na mwenzio nae ana mlengo wake mwisho kabisa ni NANI ASHINDE MGONGANO HUO.
Mtu anakuja kwako akijadili juu ya UPENDO na kwakuwa ndo hitaji la wengi unajikuta umesahau mambo ya muhimu kuja kushituka mshajenga nyumba🏠 Mnamiliki shamba🏝️ mna watoto👨‍👩‍👧‍👦 UNAANZAJE KUMUACHA KAMA SIO KUISHI NAE KWA MAJUTO MENGI KWANI MIGOGORO HAITAWAACHA SALAMA😂😂
Kabla ya kufikiria raha na amani utapata Kwenye uhusiano ama ndoa yako, tafakari kwa kina JUU YA MALENGO YAKO kwa sababu hayo ndo maisha, Starehe ya ngono 👙ipo na itakuwepo lakini ukiisha haribu msingi wa MALENGO YAKO NIAMINI UMEHARIBU MAISHA YAKO💯
Lazima umjue Mwenza wako ana malengo gani?
Unaolewa ama kuoa Mtu ambaye yeye akipata chakula, akalala pazuri, na kuweza kuvaa vizuri yeye kamaliza 😂
Wakati huo wewe unatamani kuwa mwenye nafasi kubwa ki maisha wallah hiyo ndoa ITAKUJUTISHA.
#Elista_kasema_ila_sio_Sheria 🔨
UTAMUZAIDIAPP


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/05/kila-ndoa-ina-malengo-yake-tatizo-kuu.html

No comments:

Post a Comment