Sunday, May 31, 2020

SOMA HII MDAU UTAJIFUNZA JAMBO

Utamuzaidiapp
Biology inasema, baada ya tendo la ndoa mbegu za kiume zinazoingia kwa mwanamke ni takribani mbegu milioni mia tatu(300,000,000) na zote huanza kuogelea kuelekea kwenye ovum (yai).

Kati ya hizo mbegu milioni 300 zinazofanikiwa kufika sehemu husika kwenye yai ni mbegu 500 tu, nyingine huchoka mapema na kufa njiani.
Vilevile katika hizo mbegu 500 zilizofanikiwa kufika kwenye yai ni mbegu moja tu ndiyo hushinda na kuingia ndani kutengeneza kiumbe!
*Mbegu hiyo ni wewe unayesoma ujumbe huu...*
Biology inatuambia kuwa ulikimbia mbio na kuwashinda wenzio milioni 300 na ndiyo maana leo hii upo duniani...

Usingekuwa mshindi katika mbio zile leo usingekuwepo duniani...
*Je, umeshawahi kufikiri juu ya hili!?*
Ulikimbia bila macho, mikono wala miguu na ukashinda!
Ulikimbia bila elimu yako, ujuzi wala vyeti na ukashinda!
Ulikimbia tena bila msaada wa mwingine yeyote na ukashinda...

*Ni kitu gani leo cha kukufanya uwaze kushindwa katika maisha kiasi cha kukata tamaa!?*
Sasa unayo macho, mikono na miguu,
Una elimu, ujuzi na maarifa zaidi unaongozwa na maneno ya Mw. Mungu...
kwanin uwaze kushindwa!?

*Tafakari, weka malengo, muombe Mungu kisha pambana!*
Ulizaliwa ukiwa mshindi usiishi maisha ya kushindwa!! *wewe ni shujaa💪🏾💪🏾💪🏾💪🏾💪🏾💪🏾

*SHARE UJUMBE HUU TAFADHALI


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/05/soma-hii-mdau-utajifunza-jambo.html

No comments:

Post a Comment