Saturday, May 23, 2020

NAFASI YA UPENDO NI MARA MOJA TU⚠

Chuo cha Mapenzi Kitandani - Photos | Facebook
Wala usiudanganye MOYO wako kwamba baada ya kuharibu mwanzo kuna wakati mwingine UPENDO UTAJIRUDIA
Kupenda ni matamanio ya NAFSI na kwa maana hiyo uonapo kupendwa na Mtu lakini wewe kwa NAFSI yako humpendi basi usijaribu kuja kufikiria kumpa nafasi wakati mwingine.
Kawaida ya UPENDO ni pale nafsi inapowiwa, lakini kadiri siku ziendavyo na Mtu kuona kama hapendwi na Mtu aliyegusa NAFSI yake taratibu hukata tamaa na kuendelea na maisha mengine huku akiugulia kumkosa mtu huyo, Janga hili huwapata zaidi WANAUME kwa sababu wao ndo watongozaji, Kuna ka tabia kapo kwa WANAWAKE wachache, Yaani HAMPENDI MTU ila anaweza kutamani kuwa nae, Kwa sababu hiyo akajikuta anatunza mawasiliano ya Mtu huyo kwamba SIKU AKIUMIZWA NA ALIYENAE basi atamtafuta yule ambaye alimsumbukia zamani, Na kwa taarifa yako HAKUNA MWANAUME ATAONA FULSA YA UTAMU akadengua, Wanaume kuonja ni JADI yao hivyo ATAKUTAFUNA TU mambo ya ulimkataa atayajua akiisha kuwa AMEPUMUA.
Kama humpdendi MTU usijaribu kumpa nafasi wakati ambao tayari alikuwa hakuwazii tena
Maana ukijaribu kumpa nafasi mtu ambaye tayari anae mwingine au alivunjika moyo kwako PENGINE AKUINGIZE KWENYE ORODHA YA ALIOWAHI KUWA NAO au pengine ajaribu aone una kipi cha ziada😅😅
Maana UPENDO juu yako alikuwa nao zamani na wewe ukamkataa sasa usiamini katika UPENDO WA KUDUMU
Maana wanaume UPENDO wao unaendana na mfumo dume mwisho kabisa atakuuniza kwa kulipiza MAUMIVU yale ulimuumiza wakati ule amekupenda na wewe ukadengua💃
Wanawake acheni KUFUKUA MAKABURI kwa sababu unapomuweka Mwanaume kama WA AKIBA kwamba uliye nae akizingua unamtafuta mwingine HUKO NI KUZIDI KUONA WANAUME WANA TAMAA kumbe wewe ndo umemfanya AKUPITIE KAMA UPEPO😅😅😅
Kama HUMPENDI usimpe nafasi hata ya kumsikiliza wala usimpe nafasi ya kuwasiliana nae kwa kufanya hivyo UTAJITENGA NA KINYONGO CHA WANAUME.


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/05/nafasi-ya-upendo-ni-mara-moja-tu.html

No comments:

Post a Comment