Thursday, May 21, 2020

TABIA BAADHI ya WANAWAKE ( sio rasmi)


👉1.Mke sherehe *(party wife)*
Hawa muda wote wanawaza sherehe na starehe tu, utawasikia kesho sendoff mara kitchen party .
Wako tayari kutumia hela ya chakula kwa ajili ya kuchangia sherehe.
👉2.Mke kamusi *(dictionary wife)* Hawa ni aina ya wanawake ambao huamini mawazo yao tu huwa hawapendi kushauriwa na ni wabishi sana ,huwa hawajali hata mme wake anasema nini
👉3.Mke pampas *(pampas wife)* Hawa ni wavivu sana na wamearibiwa na familia zao hasa familia tajiri, hawawezi fanya kazi wanatuma hovyo hata waume zao utasikia baby nipe hicho ,baby njoo unitolee hiki
Kama kuna house girl au boy ni zaid ya punda kwao
👉4.Mke ofisi
*(The office wife)* Hawa husahau kabisa majukumu yao kwa kisingizio ya kazi ,wanajifanya bize muda wote kuwa bize na majukumu ya kiofisi kuliko haata familia hasa mme mara nyingi hawa wanaibiwaga waume zao na mahouse girls.
👉5.Mke mgonjwa
*(Sick wife)*
Hawa muda wote ni wachovu na wanyonge ,utasikia akilalamika kuumwa huku hawaendi hospitali .
Na wanalawama kama nini usiombe ukutane naye utajuta.
👉6.Mke mwalimu mkuu
*(Headmistress)* Hawa ugeuka vilanja ndan iya familia hata mbele ya mme wake anajifanya muelekezi tu na huuliza maswali kwanini hii hivi mara hicho hivyo pasipo kujali kuna nani hata kama kuna mgeni.
👉7.Mke ngumi
*(Fighting wife)* Hawa muda wote ni wavarangati na akiamua kulianzisha huwa hawaangaliii mazingira na ataongea bila mipaka na kama unaishi uswazi kila jilani lazma atajua kumeharibika, yuko ladhi kukunjana na mume wake.
👉8.Mke Ndoo ya taka
*(Dustbin wife)* Hawa huwa wachafu kupita kiasi hawajali hiki cha thamani au vipi ,utamkuta mchafu muda wote ni mara chache kutokelezea labda kwenye sherehe. Mara nyingi waume zao wanawakinai mapema.
👉9.Mke mlinzi
*(protective wife)* Hawa huwabana waume zao mpaka kero,hujifanya wana wivu ,wanawaona wanawake wote kama maadui na hawataki hata kuona rafiki yake akiwa karibu na mume wake.
Anahisi anaibiwa ukirudi nyumbani badala ya kupokea mzigo mkononi anakupokea simu ilioyoko mfukoni .
👉10.Mke mzuri
*(Agood wife)*
Hawa ndo wale walioandikwa kwenye
*MITHALI 31* na vitabu vingine vya ndani Ya Biblia, hawa ni wapole wanyenyekevu , wasikivu hata kama amekosewa anatumia busara kulitatua tatizo,
Hawa si wengi sana katika dunia ya leo.
Mungu wabariki wanawake wote walioko namba 10 kama hawajaolewa wajaalie wapate waume bora.


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/05/tabia-baadhi-ya-wanawake-sio-rasmi.html

No comments:

Post a Comment