Ziko ndoa nyingi sana pengine napata ujasili kuitaja asilimia 85 wanawake wanaishi kuitunza heshima yake, kulinda watoto wake, kuogopa kuanza mikiki mipya ya mapenzi, Na wengine fikra zao kutawaliwa na wazo kwamba wao tena sio wanawake wanaoendana na kipindi kilichopo Yaani kwa lugha fupi ANAJIONA AMEPITWA NA WAKATI๐๐ฟโโ
Ni kweli kabisa MWANAMKE NDIYE MLINZI NA MTETEZI WA MAHUSIANO/NDOA Kwani Mwanamke akivunjika moyo wa kuendelea mara nyingi PENZI HUFA... Ziko ndoa nyingi Mama na Baba wanatoka geti moja but huko ndani hawali meza moja wala kulala chumba kimoja achilia mbali kitanda kimoja wala wasikumbuke ni lini ilikuwa mwisho kukumbatiana๐
Hatuwezi kushindwa kuwakosoa wanawake lakini tujue jambo moja ili wakati tunamkosoa Mwanamke tumpe haki yake, Mwanamke akipewa nafasi ya kuelezea kinachomuumiza mara nyingi hujisikia AMANI hata kama majibu ya upande wa pili yatakuwa YA KUMPUMBAZA ILI SIKU ZIENDE๐คฃ
Kwa maana hiyo unagunduwa kwamba kosa liko kwa MWANAUME KUSHINDWA KUTOA NAFASI YA KUMSIKILIZA MKEWE na ukifuatilia utabaini kwamba WANAUME TUNAPEANA UJINGA WA JINSI YA KUISHI NA WAKE ZETU๐ซ
Mwenzio ameoa KAHABA na Wewe umemtoa Mke wako kwenye Maadili UTAWEZAJE KU-COPY TREATMENT KWA TOFAUTI HIYO? Ukijua KUTONGOZA basi rafiki yangu ujue na KUBEMBELEZA๐
Wanawake ni watu wazuri sana ukiweza kucheza na akili yake, imagine unakutana nae barabarani unamtongoza na anaanguka kwenye himaya yako UNASHINDWAJE KUMFANYA AWE WAKO MILELE BILA KUMKOSESHA FURAHA? Nadhani na ninyi wanawake hebu wachunguzeni hao wanaume mnakutana nao, Maana bora akuombe uroda๐ tu na asikutajie NAKUPENDA! Maana najua mnako kaugonjwa ka KUPUMBAZIKA KWA MANENO MATAMU ๐ sasa rafiki sio kila neno tamu lina sukari, Wapo wanayatoa maneno matamu juu juu ila chini ya uhalisia ni kuchungu hatari๐
Nadhani tubadili mfumo wa MAPENZI tutoke kwenye NAKUPENDA na twende kwenye NAKUTAKA๐คฆ๐พโโ
Maana neno NAKUPENDA kwa sasa linatumika kama JOJO kwamba ukianza kuitafuna ni tamu but unajua mwisho wake utakuwa UMEFYONZA SUKARI YOTE mwisho wake ni kufanyaje? Sema KUTEMAAA๐๐ปโโ
Wanawake niwape mbinu๐คท๐ฝโโ
Kabla ya kumpenda mtu nawe mkubali kwa sekta ya kutimiza haja ya mwili๐
Ukiona anakupenda nawe sasa chenjia gia angani๐ซ ili mwende Sawa, Mambo ya kutamkiwa NAKUPENDA unaingia kichwa, miguu, mwili, akili na MOYO bila kujua hitaji la mwenzio AKIKUBADILIKIA VIDONDA VYA TUMBO VINAKUHUSU๐โโ๐๐ปโโ
source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/04/akiogopa-ni-kuzaa-mtoto-ambaye-hatakuwa.html
No comments:
Post a Comment